Deuteronomy 28:1-6

Baraka Za Utiifu

(Walawi 26:3-13; Kumbukumbu 7:12-24)

1 aKama ukimtii Bwana Mwenyezi Mungu wako kwa bidii na kufuata amri zake zote ninazokupa leo kwa bidii, Bwana Mwenyezi Mungu wako atakuweka juu ya mataifa yote katika dunia. 2 bBaraka hizi zote zitakuja juu yako na kukupata, kama ukimtii Bwana Mwenyezi Mungu wako:

3 cUtabarikiwa mjini na utabarikiwa mashambani.

4 dUtabarikiwa uzao wa tumbo lako, na mazao ya nchi yako na wanyama wako wachanga wa kufugwa, yaani ndama wa makundi yako ya ng’ombe, na wana-kondoo wa makundi yako.

5Kapu lako na vyombo vyako vya kukandia vitabarikiwa.

6

eUtabarikiwa uingiapo na utabarikiwa utokapo.

Copyright information for SwhKC